Jumatano, 18 Novemba 2015

Tanzania Daima Mwanza mipango mkakati



PUBLISHERS OF TANZANIA DAIMA AND SAYARINEWPAPERS
MKWEPU STREET. BILICANA'S BUILDING 1ST FLOOR.
P.O.BOX 15261 DAR ES SLAAM, TANZANIA.
TEL: 022 2126233, FAX 022 2126234
EMAIL: tzdaima(£)freemedia.co.tz
Kumb Na. FML/Adv/VOL.007/2015 Tarehe: 29/09/201!
Ndugu,
YAH: TOLEO MAALUMU LA MKOA WA MWANZA
Tafadhali husika na somo tajwa hapo juu lajieleza.
Kampuni ya Free Media Ltd inayochapisha kila siku magazeti ya Tanzania Daima na Sayari na
kusambazwa nchi nzima, inakusudia kuchapisha toleo maalumu kwa ajili ya kutangaza miradi
mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na taasisi, makampuni na mashirika ya umma na sekta
binafsi Mkoa wa Mwanza.
Toleo hili maalumu litachapishwa kwenye gazeti la Tanzania Daima na kusambazwa nchi nzima
mwezi Novemba 26, 2015. Miradi yote ya maendeleo ndiyo tunayokusudia kuitangaza kwenye toleo
maalumu kutoka mashirika, kampuni na taasisi za umma na sekta binafsi.
Pia kampuni, taasisi na shirika lolotc litakalotupa tangazo/matangazo tutaiandikia makala bure ya
utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Makala itatoka siku hiyo hiyo ya toleo maalumu (Yaani tutatoa
tangazo lako na makala kwenye ukurasa unaoruata) katika gazeti la Tanzania Daima.
Kwa hiyo, ukiwa mdau wa maendeleo Mkoa wa Mwanza unaombwa na kukaribishwa kutangaza
utekelezaji na mikakati ya shughuli za maendeleo kutoka taasisi, kampuni na shirika lako kwa
manufaa ya Taifa.
Hi kufanikisha azma hii, tunakuomba ushirikiano wako wa dhati katika toleo hili maalumu. Ahsante n
karibu sana.
Gharama zetu za matangazo ni kama ifuatavyo;
Ukurasa mzima „.1,925,000/=
Nusu Ukurasa 962,500/=
Robo Ukurasa 495,000/=
Bei hizo ni bila Ongezeko la Thamani yaani (VAT)
Wasiliana na Sitta Tumma, Mkuu wa Tanzania Daima Kanda ya Ziwa.
Twalib Mungulu
Meneja Matangazo
Simu: 0713 296570 au 0767296570

Alhamisi, 20 Agosti 2015

Watu wanane wafariki ajali ya gari





Watu wanane wafariki ajali ya gari

By CHARLES MSETI

WATU wanane wamefariki dunia na wengine sita kujeruhiwa  katika ajali ya gari yenye namba za usajili T. 812 BJU Toyota Noah, iliyokuwa ikitoka Shinyanga kwenda mkoani Geita.

Ajali hiyo imekuja ikiwa wimbi la ajali za barabara likiwa limepungua baada Machi 11 mwaka huu wilayani Mufinga, Iringa watu  50 kufariki na kufanya katika kipindi hicho kutokea ajali kubwa nane zilizosababisha vifo vya watu kadhaa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishina Mwandamizi Msaidizi, Charles Mkumbo, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, huku akisema tukio hilo lilitokea juzi saa 11 jioni katika Kijiji cha Mwamanga, Misungwi mkoani hapa.

Mkumbo alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa gari ambao ulisababisha dereva wa gari hilo ambaye hajafahamika jina lake mpaka sasa kushinda kulimdu kuliongoza na kupindu. 

 Kamanda Mkumbo aliwataja watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo kuwa ni, Malongo Magongo, Yun Somanga, Shija Somanga, Thobias Simon, Michael Simon, Amos Lukenza, Shaban Deus na Samwel Malongo wote wakiwa ni wakzi wa Geita.

“Majina ya majeruhi hao ni John Nyahunga, Charles Ludahula (mkazi Sengerema), Elias Mkenza, Shija Magongo, Simon Lukenza na Malongo Samwel, wakazi wa Geta na miili yao imelazwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando (BMC),” alisema Mkumbo.

Katika hatua hiyo Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, limetoa onyo kali kwa madereva wa mabasi makubwa ya abiria na za watu binafsi kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali zisizokuwa za lazima ambazo zinasababisha kukatisha uhai wa binadamu.




Jumatano, 19 Agosti 2015

Mwenyekiti Halmashauli ajivunia maendeleo chini ya Chadema



Mwenyekiti Halmashauli ajivunia maendeleo chini ya Chadema


 By Tza Repoter


MWENYEKITI wa Halmashauli ya Wilaya Ukerewe, Joseph Mkundi, amejivunia maendeleo aliyofanya katika kipindi cha uongozi wake, ikiwemo mradi wa maji uliogharimu billioni 6, huduma ya afya, miundombinu ya barabara na sekta ya elimu.


Kauli hiyo aliitoa juzi mbele ya waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu ya Serikali ya kugombea ubunge katika jimbo hilo, lililokuwa linaongozwa na Salvatory Machemli, analiemaliza muda wake kabla ya kuangukia pua katika kura za maoni.


Mkundi ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Bukiko Chadema, alisema katika kipindi cha miaka mitano, Halmashauli hiyo ikiwa chini ya Chadema wamefanikiwa kutatua kero za Wananchi ambazo zilikuwa ni sugu ikiwemo barabara na afya zilizokuwa zikisababisha kina mama wajawazito kujifungulia njiani.


Alisema endapo atafanikiwa kuwa mbunge, atahakikisha anatatua miradi ya maendeleo ambayo haijakamilika ikiwemo barabara na vituo vya afya ambavyo awali wananchi walikuwa na shauku ya kuona vituo katika kata na kijiji.


Alisema waliweza kushirikiana vyema na Machemli katika uongozi wao kuwarahisishia wananchi huduma ya afya, kushukua kwa gharama za matibabu kwa wazee na watu wasiojiweza kutibiwa bure.

“Tukiwa bado tunapambana na afya na miundombinu ya barabara, bado Wilaya ya Ukerewe kuna changamoto nyingi ikiwemo ya wavuvi na asilimia kubwa ya watu wanaoishi hapa wanategemea uvuvi hivyo kuna kila sababu kazi hii kutambulika kama kazi nyingine.


“Endapo kama tukiwabadilisha hawa wavuvi wetu na wakatambulika ni kama nyingine ni imani yangu tutakuwa tumeokoa Taifa hili na ni malengo yangu nikiwa mbunge wa hapa wavuvi hawa ni wa kuwasaidia,” alisema  mkundi.


 Mkundi alisema katika Wilaya hiyo licha ya kutegemea uvuvi pia imejaliwa kuwa na matunda aina ya machungwa ambayo yamekuwa yakiozea shambani, hivyo akifanikiwa kuwa mbunge hiyo ni moja ya mikakati ya kutafuta wawekezaji watakaoweza kununua matunda hayo.


Alisema umefika wakti wa Wananchi kukiogopa Chama cha Mapinduzi (CCM) kama ugonjwa wa ukoma kutokana na ahadi zao, hewa na zisizokamilka na badala yake wanapaswa kuwachagua wabunge wa Ukawa katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.



Jumatano, 12 Agosti 2015

Katibu CCM atwangwa na wanachama



Katibu CCM atwangwa na wanachama

By Charles Mseti

HALI isiyokuwa ya kawaida Wanachama na wafuasi wa Chama cha Mapinduzi (CCM)  Kata ya Bugogwa Mkoa wa Mwanza wamevamia na kumtembezea kichapo, Katibu wa chama hicho Wilaya ya Ilemela, Acheni Maulid, kwa madai ya kushindwa kurejesha jina la mshindi katika kura za maoni, Maliki Hatib.

Tukio hilo limekuja ikiwa ni mwendelezo wa matukio ya aina hiyo kutokea hapa nchini wakati wa kura za maoni ndani ya Chama hicho, ambacho kimeonekana kugubikwa na vitendo vya vurugu na kupingwa matokeo.

Tukio hilo limetokea jana saa tano asubuhi katika ofisi za CCM zilizopo eneo la Maliasili Pasiansi, wakati wanachama hao zaidi ya 30 walipoandama mpaka ofisini hapo kwa lengo la kutaka kufahamu chanzo na sababu za kukatwa kwa mshindi huyo.

Msetiblog, imeshuhudia wanachama hao waktoa kichapo kwa katibu huyo wakirusha ngumu na mateke huku wakimtoa nje ya Ofisi hiyo kabla ya Askaari Polisi kufika eneo hilo na kuanza kupiga risasi za machozi juu.

Hata hivyo licha ya Askari Polisi hao kupigia risasi za machozi hewani kwa lengo la kuwatuliza na  kuwatawanya wanachama na wafuasi hao,bado waliendelea kufanya fujo zilizodumu takribani saa nne ambako Polisi walifanikiwa kumkamata mfuasi mmoja ambaye hakufahamika jina lake kitendo kilichotuliza kasheshe hilo.

Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Bugogwa, January Samamba na Mwenyekiti wa Kata hiyo, Amos Samwel, kwa pamoja wamesema kitendo cha viongozi wa chama hicho kushindwa kurudisha maji ya watu wanaokubalika kutasababisha kishindwe katika uchaguzi wa Mwaka huu.

Walidai kuwa kamwe hawatakubali kuona haki ya mtu ikipotea na wakafumba macho na kwamba endapo viongozi wa ngazi ya juu watalazimisha kupitisha jina la Steven Mashamba, ambaye alikuwa mshindi wa pili aliepata kura 597 ,watapigia kura vyama vya upinzani.

“Kama watampishia huyo wanaemtaka wao kwa kisingizo kwamba, Hatib  ni mkimbizi  kuwa sio mtanzania watampigia kura wao wenyewe sisi hatutapiga kura na tutawashawishi watu wengine kupigia upinzania,” wamesema.

Akizungumza na mara baada ya kutulia kwa fujo hizo, Katibu wa Wilaya hiyo, Acheni Maulidi, amesema chanzo cha kukatwa jina mshindi huyo ni kutokana na uraia wake kuwa shaka hivyo wasingeweza kumpitisha.

Amesema mara baada ya kura za maoni kumalizika na majina kupelekwa mkoani, walianza kuyapitia majina yote ambako mshindi huyo alitiliwa shaka na uraia wake na kumtaka kupeleka vyeti vya kuzaliwa na kwamba alishindwa kufanya hivyo.

“Sisi baada ya kuutilia shaka uraia wake tulimwambia alete vyeti vyake vya kuzaliwa lakini sasa alishindwa kufanya hivyo na mpaka siku ya mwisho tulisikia ameenda mahakamani, tusingeweza kupitisha mtu wa aina hiyo,” amesema Maulidi.

Mshindi wa matokeo hayo, Maliki Hatib, amesema kitendo cha viongozi wa CCM kushindwa kurudisha jina lake kitasababisha chama hicho kuacha kuchaguliwa na kuchukiwa na Wananchi na kwamba yeye ni raia halisi wa Tanzania.

Jumatano, 5 Agosti 2015

Wagombea 10 ccm wapinga matokeo ubunge Mwanza



Wagombea 10 ccm wapinga matokeo ubunge Mwanza

By Charles Mseti

JUMLA ya wagombea10 kati ya 20 walioshindwa kwenye kura za maoni ndani ya  Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika jimbo la Nyamagana Jijini Mwanza, wameandika waraka mzito wa kupinga matokeo, yaliyompa ushindi Meya wa Jiji la Mwanza, Stanslaus Mabula.

Wagombea hao wameandika waraka unaolalamikia matokeo ya uchaguzi huokwamba haukufanyika kwa haki na huru kutokana na kutawaliwa na vitendo vya rushwa vilivyokuwa vikifanywa na meya huyo.

Waraka huo ulioandikwa na wagombea hao umetumwa kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdurlahiman Kinana na nakala yake kutumwa kwa Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Phillip Mangula, Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Mwanza, Dk. Anthony Diallo, Katibu wa Mkoa, Miraji Mataturu na Mkuu wa Mkoa, Magesa Mulongo.

 Wagombea hao ni kati ya wanachama 20 wa CCM walijitokeza kuingia katika kinyang’anyiro hicho akiwamo, Mabula ambaye alitangazwa  mshindi baada ya kupata kura 3,553 akifuatiwa na Joseph Kahungwa, kura 3,647 na Raphael Shilatu (kura 864).

Waraka huo ambao ulioandikwa Agosti 2, mwaka huu na kusainiwa na wagombea hao, unaeleza uchaguzi huo wa kura za maoni katika jimbo hilo, uligubikwa na vitendo vya rushwa, ulaghai, dhuluma na ukiukwaji wa taratibu na kanuni za uchaguzi.

Hata hivyo  malalamiko hayo yameelekezwa kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana, Elias Mpanda na Mabula ( Diwani wa Kata ya Mkolani), aliyemaliza muda wake Julai 8, mwaka huu.

Waraka huo umeandikwa na wagombea 10 kama yanavyosomeka hapo ni Stephen Deya, Robert Masunya, Raphael Shillatu, Joseph Kahungwa, Tumaini Lusenga, Wisandara Muhindi, Komanya Kitwala, Dede Petro, Aviasi Said na Tausi Halili..

Pia wagombea hao wanadai na kumtuhumu Katibu huyo wa CCM  wa Nyamagana kwamba alitumia lugha kali na vitisho vilivyowanyima wao fursa na  uhuru wa kujieleza kwa wapiga kura na kumpatia muda mwingi wa kujieleza.

Wanadaiwa kuwa baadhi ya wapiga kura walikutwa na kadi bandia ambazo walizikabidhiwa kwa katibu huyo ambaye hata hivyo inadaiwa hakuchukua hatua zozote dhidi ya wahusika.

Kwa mujibu wa wagombea hao, madaftari mengi kwenye matawi yalikuwa na majina ya wanachama wapya pekee, huku wa zamini majina yao yakiwa hayaonekani ,hali iliyosababisha wanachama wa muda mrefu kupinga uchaguzi huo katika baadhi ya vituo baada ya kunyimwa fursa na haki ya kupiga kura.

Matawi yaliyokuwa na tatizo hilo ni  Maswa Magharibi, Isagenghe, Unguja, Ndofe, Nyamagana, Mwananchi – Tandabui na Nyakabungo, wengi wa wanachama  wakiwamo wajumbe wa mashina ( mabalozi), wenyeviti wa mtaa na baadhi ya wagombea udiwani majina yao hayakuonekana kwenye vitabu, hivyo kunyimwa fursa ya kupiga kura.

“Vituo viwili vilivyorudiwa uchaguzi vilifungwa mapema, ambavyo ni Isagenghe kilichofungwa saa 8:00 mchana na Maswa Magharibi kilichofungwa saa 7:30 mchana.Licha ya kuridiwa kwa uvhaguzi,hatukishirikishwa,”

“Uchaguzi katika matawi ya Isagenghe na Maswa Magharibi uliahirishwa na kisha kufanyika siku iliyofuata Jumapili Agosti 2/8/2015 bila wagombea kupewa taarifa na hii imefanyika ili kutoa mwanya kupigwa kwa kura isivyo halali bila mawakala wa wagombea kuwapo vituoni.

“Tumeshuhudia watu wanakuja kupiga kura wakiwa na maelekezo ya kumpigia mgombea ndugu Mabula kutoka kwa mwanachama aliyekiri kuwa ni mtu wa Mabula,” inaeleza sehemu ya waraka huo ( nakala yake tunayo)

Malalamiko mengine yanaeleza kwamba lilikuwapo kundi la vijana wenye umri wa chini ya miaka 14 walioandaliwa kumpigia kura Mabula kwa kutumia kadi za CCM kutoka jimbo jirani la Ilemela.

Inadaiwa katika warka huo kuwa, mmoja wa vijana hao amekiri kumpigia kura Mabula kwa kadi hiyo ambyo imetumika zaidi ya mara moja katika kituo kile kile cha Isagenghe. Kadi hiyo ni namba AF 5590765 iliyotolewa tarehe 25/10/200.

Kuhusu rushwa, wanadai wana ushahidi wa kuthibitisha jinsi Mabula alivyogawa fedha kwa vijana 30 ili wampigie kura ya maoni na  baadhi yao waliruhusiwa kupiga kura bila kuwa na kadi za chama,pia alitumia gari T.151 DAY aina ya Noah,kugawa rushwa kwa wapiga kura, iliyopewa jina la gari la BOT.

“Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye ni Katibu wa Wilaya (Mpanda) ameonyesha upendeleo kwa ndugu Mabula tangu kipindi cha kampeni na upigaji wa kura za maoni kwani alionekana kupewa upendeleo wa muda wa kutosha kujinadi kuliko mgombea yeyote.

“Kwa misingi hiyo, hatukubaliani na matokeo hayo na hatuungi mkono juhudi zozote za kumpitisha Mabula aliyeonekana kuhujumu maslahi mapana ya chama na kuharibu mshikamano wa wagombea wenzie na wanachama kwa ujumla.

“Ombi letu, tunaomba busara za chama zitumike ili kukomboa jimbo letu kutoka kwa wapinzani kwa kupata mgombea safi asiyekuwa na wasifu wenye madoa, anayekubalika ndani na nje ya chama,” wanaeleza wagombea hao katika waraka huo.

Juhudi za kumpata Mabula ili  kuzungumzia sakata hilo, hazikuzaa matunda baada ya gazeti hili kumpigia simu yake ya mkononi iliita bila kupokelewa na mara nyingine haikupatikana.

Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana, Elias Mpanda, juhudi za kumpata kiongozi huyo kujibu malalamiko hayo licha ya mwandishi wa habari hizi kwenda ofisini kwake hakumkuta hata alipopigiwa simu yake ya mkononi haikuwa hewani.

Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Miraji Mtaturu,  alipoulizwa alikiri kupokea malalamiko ya wagombea hao wanaopinga matokeo ya kura ya maoni ya ubunge katika Jimbo la Nyamagana na kuongeza kuwa karibu matokeo katika majimbo yote ya mkoa wa Mwanza yamelalamikiwa.

“Malalamiko hayo si Nyamagana pekee, kuna, Ilemela, Magu na Kwimba yote yanalalamikiwa,Watu wanajenga dhana kuwa wanaposhindwa wanalalamika kuwa hawakutendewa haki,” alisema Mtaturu.

Mtaturu alisema ofisi yake haiwezi kuzuia mamlaka ya juu ya chama hicho na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuendelea na mchakato wa kupitia na kuthibitisha majina ya wagombea ubunge hadi hapo itakapojiridhisha kuwa malalamiko hayo ni kweli.

mwisho